Get Paid To Promote, Get Paid To Popup, Get Paid Display Banner

WAZIRI MAGHEMBE AKABIDHI VISIMA 20 VILIVYOKARABATIWA NA TBL WILAYANI MISUNGWI

Posted by dani handrian
 Meneja Mauzo wa Kampuni ya Bia Tanzania  (TBL) wa mikoa ya Simiyu, Mwanza  na Mara, Josephat Changwe, akimwongoza Waziri wa Maji , Profesa Jumanne Maghembe (kulia) kuzindua moja ya visima 20 vya maji salama ya kunywa vilivyokarabatiwa na kampuni hiyo kwa gharama ya sh.49.5 milioni, wilayani Misungwi,Mwanza juzi.Anayepiga makofi (kushoto) ni Mbunge wa jimbo la Misungwi, Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais-Mazingira, Charles Kitwanga.
 Waziri wa Maji, Profesa Jumanne Maghembe (kulia), Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais,Mazingira ambaye pia ni Mbunge wa Misungwi, Charles Kitwanga (wa tatu kulia) na Meneja Mauzo wa Kampuni ya Bia Tanzania  (TBL) wa mikoa ya Simiyu, Mwanza  na Mara, Josephat Changwe wakisaidia kumtwisha dumu la maji mmoja wa wanawake wa Kijiji cha Mapilinga, Wilaya ya Misungwi, ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa moja kati ya visima 20 vilivyokarabatiwa na TBL wilayani humo, kwa sh. mil 49.5.
 

Copyright © 2009 ikpopped | Design by [blogger merak dua]